Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa wakati huu wa nyuma, jua, mwangaza, mwezi na nyota hazionekani tena, mawingu yanarudia nyuma ya mvua,

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 12:2
15 Referans Kwoze  

Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli kama uvumi wa bahari iliyochafuka. Atakayeiangalia inchi kavu ataona giza tupu na taabu, mwangaza utafunikwa na mawingu.


Huyo mutu alipotaja tu Sanduku la Mungu, Eli alianguka machali kutoka kwenye kiti chake pembeni ya mulango. Eli alipoanguka hivyo, shingo yake ilivunjika maana alikuwa muzee na munene, naye akakufa. Eli alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka makumi ine.


Wakati huo, Eli alikuwa na umri wa miaka makumi kenda na nane na macho yake yalikuwa yamepofuka.


Kwa mukono wako wa kuume uliwakomboa watu wako; uliwakomboa wazao wa Yakobo na Yosefu.


Umeniletea taabu kubwa, lakini utanirudishia tena uzima, wewe utaniinua tena kutoka katika shimo.


Roho yangu imeregea kabisa, kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu, kutoka katika eneo la Yordani, kutoka mulima Hermoni na Mizari.


Siku moja usiku, Eli ambaye macho yake yalikuwa yamefifia, alikuwa amelala katika chumba chake.


Macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee. Basi, Yosefu akasogeza wana wake karibu na baba yake, naye akawabusu na kuwakumbatia.


Na ilikuwa wakati Isaka alipokuwa muzee na macho yake yalikuwa zaifu hata hakuweza kuona tena, akaita Esau mwana wake mukubwa, akamwambia: “Mwana wangu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


Muda wa maisha yetu ni miaka makumi saba, au tukikuwa wenye afya, miaka makumi nane; lakini yote ni shida na taabu! Siku zinapita mbio, nasi tunatoweka!


Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite