Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 12:1
40 Referans Kwoze  

Ni vizuri kwa mutu kujifunza uvumilivu tangu wakati wa ujana wake.


Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Umufundishe mutoto njia anayopaswa kufuata, naye hataiacha hata katika uzee.


Lakini Yesu akawaita na kusema: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.


Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.


Tena, tangia utoto wako unajua Maandiko Matakatifu yanayoweza kukupatia hekima kusudi uokolewe kwa njia ya kumwamini Kristo Yesu.


Muda wa maisha yetu ni miaka makumi saba, au tukikuwa wenye afya, miaka makumi nane; lakini yote ni shida na taabu! Siku zinapita mbio, nasi tunatoweka!


Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Lakini Barzilayi akamwambia mufalme: “Niko tena na miaka mingi ya kuishi ndipo niende nawe mufalme mpaka Yerusalema?


Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


kwa maana atahesabiwa kuwa mutu mukubwa mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kinywaji kikali, na atajazwa na Roho Mutakatifu tangu kuzaliwa kwake.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.


Na ninyi wababa musiwakasirikishe watoto wenu. Lakini muwalee na kuwaonya, mukiwatolea mashauri yanayotoka kwa Bwana.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Ninaogopa kwamba mara tu nitakapoondoka, Roho wa Yawe atakunyanyua na kukupeleka pahali nisipopajua! Nikienda kumwambia Ahabu kwamba uko hapa, naye akikutafuta na asikupate, ataniua mimi, ingawa mimi mutumishi wako ninamwogopa Yawe tangu ujana wangu.


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


Wageni wamenyonya nguvu zake, wala yeye mwenyewe hajui; imvi zimejaa juu ya kichwa chake, lakini yeye mwenyewe hana habari.


Ningepata faida gani katika mikono yao, watu ambao nguvu zao zilikuwa zimewaishia?


Watu wote wa Israeli watafanya kilio na kumuzika. Lakini, ni huyo tu wa jamaa ya Yeroboamu atakayezikwa, maana ni yeye tu wa jamaa ya Yeroboamu aliyepata kupendezwa na Yawe, Mungu wa Israeli.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


Roho yangu itafurahi kama mwenye kushiba minofu yenye mafuta, kwa shangwe nitaimba sifa zako.


Usiku ninakukumbuka, ee Yawe, na kushika sheria yako.


Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.


Mimi leo nina umri wa miaka makumi nane. Niko na uwezo wa kutambua yanayokuwa mazuri na yale yasiyokuwa mazuri? Mimi mutumishi wako ninaweza tena kutambua onjo ya kile ninachokula au kunywa? Nitaweza tena kutambua uzuri wa sauti za waimbaji wanaume au wanawake? Kwa nini mimi mutumishi wako nikuwe muzigo wa zaidi kwako bwana wangu mufalme?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite