Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 11:2
22 Referans Kwoze  

Kuna vitu sita Yawe anavyochukia, hata saba ambavyo ni chukizo kwake:


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Atakuokoa mara sita toka katika magumu; hata mara saba hasara haitakugusa.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Muwakumbuke wale wanaofungwa, mukijisikia sawa vile wenye kufungwa pamoja nao. Vilevile muwakumbuke wale wanaoteswa, mukijisikia sawa vile wenye kuteswa kama wao.


Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.


Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.


Kama akikukosea mara saba kwa siku, na akirudia kwako kila mara kwa kukuomba huruma, umusamehe.”


Yesu akamujibu: “Hapana, sikuambii kwamba umusamehe mara saba tu, lakini mpaka mara makumi saba mara saba.


Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


Wayuda walishinda waadui zao katika siku hizo, na katika mwezi huo huzuni yao iligeuzwa kuwa furaha, na kilio chao kuwa sikukuu. Waliagizwa wakuwe wanazikumbuka siku hizo kwa kufanya karamu na sherehe, kupelekeana zawadi za chakula na kuwapa wamasikini vitu.


Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.


Sasa murudi kwa nyumba mufanye sherehe, mukule vyakula na kunywa divai nzuri, lakini mukumbuke kuwapelekea wale ambao hawana kitu cha kutosha; maana leo ni siku takatifu kwa Bwana wetu. Musihuzunike kwa sababu furaha Yawe anayowajalia itawapa nguvu.”


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha. Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini, pale unapoangukia ndipo unapolala.


Mutu akiishi miaka mingi, afurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kwamba siku mbaya zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”


Ukiwauliza, watakuambia. Sasa ninakuomba vijana wangu hawa wapate kukubaliwa mbele yako, maana tumefika wakati wa sikukuu. Tafazali uwapatie kitu chochote unachokuwa nacho watumishi wako hawa nami mwana wako Daudi.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite