10 Ondoa mahangaiko ndani ya moyo wako, ujikinge usipate maumivu katika mwili kwa sababu ujana na nguvu vinapita mbio.
Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.
Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.
Ukumbuke Muumba wako siku za ujana wako wakati hazijafika siku mbaya wala haijakaribia miaka utakaposema: “Sina furaha katika vitu hivyo.”
Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!
Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure!
“Ee Yawe, unijulishe mwisho wangu, siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi, nijue namna maisha yangu yanavyopita upesi!”
Japo alijisikia amejaa nguvu ya ujana, lakini italala pamoja naye katika mavumbi.
Wewe umetoa mashitaki makali juu yangu, na kunibebesha zambi za ujana wangu.
Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako, kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.
Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.
Mupumbafu hawezi kuwa na maarifa. Punda wa pori ni punda wa pori tu.
Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!