3 Hata anapopita katika njia, anakosa akili, anamwambia kila mutu kwamba yeye ni mupumbafu.
Mupumbafu hapendezwi na ufahamu; kitu cha maana kwake ni maoni yake tu.
Mwenye akili anatenda kila kitu kwa kufikiri, lakini mupumbafu anatembeza upumbafu wake.
Sasa, wapagani wanashangaa kuona ninyi hamushirikiani nao tena katika maisha ya ovyo ovyo; na kwa hiyo wanawasingizia ninyi.
Ukimutolea Mungu ahadi, usikawie kuitimiza. Mungu hapendezwi na wapumbafu. Timiza kile ulichoahidi.
Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.