Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 10:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Usimutukane mutawala hata ndani ya moyo wako, wala usimutukane tajiri hata ndani ya chumba chako cha kulala, maana ndege atapeleka sauti yako, kiumbe kinachoruka kitatangaza maneno yako.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 10:20
11 Referans Kwoze  

Paulo akasema: “Wandugu zangu, sikujua kwamba yeye ni Kuhani Mukubwa. Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimulaani mukubwa wa taifa lako.’ ”


Usikawie kunitolea sehemu yangu kutokana na wingi wa mazao yako na divai yako. Mutanipa wazaliwa wenu wa kwanza wanaume.


Mumoja wao akajibu: “Hakuna anayekuwa upande wake, ee mufalme. Anayefanya vile ni Elisha, nabii anayekuwa kule Israeli. Yeye anamwambia mufalme wa Israeli mambo yote unayosema hata ukiwa katika chumba chako cha kulala.”


Yesu akawajibu: “Ninawaambia ninyi: kama watu hawa wakinyamaza, mawe yatalalamika.”


Lakini Marta alikuwa anafungwa na kazi nyingi za nyumba. Kwa hiyo akamwendea Yesu na kumwambia: “Bwana, haikuhangaishi kitu kuona jinsi dada yangu anavyoniachilia kutumika mimi peke? Umwambie anisaidie.”


Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni


Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao vilevile wakaleta vyura katika inchi ya Misri.


Usimutukane Mungu, wala kumulaani mukubwa wa watu wako.


Mordekayi akapata habari hiyo, akamujulisha malkia Esteri, naye Esteri akamupasha mufalme habari.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite