Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mambo yote yanasababisha muchoko, muchoko mukubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 1:8
16 Referans Kwoze  

Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.


Nitakushukuru maisha yangu yote, nitakuomba nikikuinulia mikono yangu.


Mito yote inatiririkia ndani ya bahari, lakini bahari haijai hata kidogo; kule ambako mito inatiririkia ndiko kule inaendelea kwenda.


Mulitazamia mavuno mengi, lakini mulipata kidogo tu. Mulipoyaleta kwenye nyumba, niliyapeperusha mbali. Kwa nini? Kwa sababu nyumba yangu ni mabomoko matupu wakati kila mumoja wenu anashugulikia nyumba yake.


Mutu anatoa jasho kwa ajili ya kupata chakula, lakini tamaa yake ya kula haitoshelezwi hata kidogo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite