Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 1:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 1:17
14 Referans Kwoze  

Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Kwa hiyo, nikachukia maisha, maana yote yanayotendeka chini ya jua yalinisikitisha. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Ni afazali kuwa na kidogo tu, pamoja na amani ndani ya moyo, kuliko kutoa jasho kwa ajili ya kukamata upepo.


Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kumata upepo. Afazali kufurahia kitu ambacho uko nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Basi, nilijaribu kufikiri juu ya jambo hili, lakini lilikuwa gumu sana kwangu,


Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.


Kila mara nilipojitoa kwa kujua hekima na kuona yanayotendeka hapa katika dunia, nilitambua kwamba mutu anaweza kukaa macho muchana na usiku,


Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite