Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Maana, mutoto mwanaume anamuzarau baba yake; mutoto mwanamuke anabishana na mama yake, muke wa mwana anapingana na mama mukwe wake. Waadui wa mutu ni watu wa nyumba yake.

Gade chapit la Kopi




Mika 7:6
24 Referans Kwoze  

Baba atapingana na mwana wake, na mwana atapingana na baba yake. Mama atapingana na binti yake, na binti atapingana na mama yake. Mama mukwe atapingana na muke wa mutoto wake, na muke yule atapingana na mama mukwe yake.”


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


Wanasema: “Magonjwa haya yatamwua; hatatoka tena ndani ya kitanda chake!”


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


Kuna watu ambao wanalaani baba zao, wala hawana shukrani kwa mama zao.


Mutatolewa hata na wazazi wenu, wandugu zenu, na watu wa jamaa zenu pamoja na warafiki zenu. Nao watawaua wamoja kati yenu.


Yesu akajibu: “Yule aliyechovya mukate pamoja nami ndani ya sahani ndiye atanitoa.


Washirika wenzenu wamewadanganya, wamewafukuza toka katika inchi yenu. Watu muliopatana nao wamewashinda katika vita. Warafiki wa kutegemewa ndio waliokutegea mitego, nawe haukuelewa yaliyokuwa yanatendeka.


Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.


Hata wandugu zako, jamaa yako mwenyewe, nao vilevile wanakudaganya; wanakukaripia waziwazi. Usiwaamini hata kidogo, ingawa wanakuambia maneno mazuri.


Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


Tena mufalme Daudi akamwambia Abisayi na hata watumishi wake wote: “Ikiwa mutoto wangu mwenyewe anayawinda maisha yangu, si ni zaidi kwa mutu wa kabila la Benjamina? Ninyi muache anilaani maana Yawe amemwagiza anilaani.


Wewe ni kama maji ya mafuriko. Lakini hautakuwa wa kwanza tena, maana ulipanda juu ya kitanda changu mimi baba yako, wewe ulikichafua; hakika wewe ulipanda juu yake!


wananyanganya upande mumoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mumoja anamushambulia mwenzake.


Kila mutu anadanganya jirani yake, hakuna hata mumoja anayesema ukweli. Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo; anatenda uovu kwa kadiri ya kushindwa kabisa kunigeukia.


Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite