Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 7:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Utatuhurumia tena; utatupilia mbali zambi zetu, utazitupa zote katika vilindi vya bahari.

Gade chapit la Kopi




Mika 7:19
36 Referans Kwoze  

Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako.


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa maana hamutatawaliwa tena na zambi, kwa sababu hamuishi chini ya uongozi wa Sheria lakini chini ya uongozi wa neema ya Mungu.


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.


Kama mashariki inavyokuwa mbali na magaribi, ndivyo anavyotenga zambi zetu mbali nasi.


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Kwa maana kama mukiishi kufuatana na hali ya kimwili, mutakufa. Lakini kama mukiua matendo mabaya ya mwili kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, mutaishi.


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Yeye atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika maovu yao yote.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Ingawa atatufanya tuhuzunike, atakuwa na huruma tena, kadiri ya wingi wa wema wake.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe atawatetea watu wake, na kuwahurumia watumishi wake, wakati atakapoona nguvu zao zimeisha wala hakuna aliyebaki, mufungwa au mutu huru.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


hapo Yawe, Mungu wenu, atawarudishia mema yenu na kuwahurumia na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa ambamo atakuwa amewatawanya.


Mimi nitawasamehe maovu yao, wala sitakumbuka tena zambi zao.”


Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa; watu watasamehewa uovu wao wote.


Nitatakasa zambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea.


Makosa yake yote aliyofanya hayatakumbukwa; kwa sababu ya haki yake ataishi.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Malaika akawaambia watumishi wake: Muvue Kuhani Mukubwa Yoshua nguo zake zenye kuchafuka. Kisha akamwambia Kuhani Mukubwa Yoshua: Nimeiondoa zambi yako, nami nitakupatia nguo za bei kali.


Daudi akamujibu Gadi: “Nina mashaka makubwa! Lakini afazali kuazibiwa na Yawe, kuliko kutiwa katika mikono ya watu, maana yeye ana rehema sana.”


Umewasamehe watu wako kosa lao; umefuta zambi zao zote.


Wema wa Yawe haukomi, huruma zake hazina mwisho.


Nitakapowajaza Waisraeli Roho yangu, sitageuka tena wasipate kuniona. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite