Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 7:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Watatambaa katika mavumbi kama nyoka, kama viumbe vinavyotambaa. Watatoka katika makimbilio yao wakitetemeka na kujaa hofu. Watakugeukia Yawe, Mungu wetu, kwa hofu, wataogopa kwa sababu yako.

Gade chapit la Kopi




Mika 7:17
27 Referans Kwoze  

Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake, wapinzani wake walambule vumbi.


Waliposikia tu habari zangu, walinitii; wageni walinijia wakinyenyekea.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Inamupasa kuinama na kujinyenyekeza, labda tumaini litakuwa likingali.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Imbwa wa pori na kondoo watakula pamoja, simba watakula majani kama ngombe, lakini chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Katika mulima wangu wote mutakatifu, hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia, ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Toka magaribi mpaka mashariki, kila mutu atamwogopa Yawe na kutambua utukufu wake. Maana atakuja kama muto wenye kuporomoka mbio, muto unaosukumwa kwa upepo wa Yawe.


Kwa hiyo watu wenye nguvu watakutukuza, miji ya mataifa kali itakuogopa.


Ee Yawe, simama sasa mwanadamu asishinde! Uyakusanye sasa hivi mataifa mbele yako, uyahukumu.


Basi, wakajitokeza kusudi Wafilistini wawaone. Wafilistini walipowaona wakasema: “Muangalie wale Waebrania wanatoka kwenye mashimo walimokuwa wamejificha.”


Wakamujibu Yoshua: “Tuliambiwa kwamba kwa hakika Yawe, Mungu wenu, alimwamuru mutumishi wake Musa awaangamize wakaaji wote wa inchi hii na kuwapa ninyi inchi hii ikuwe mali yenu. Kwa hivyo, tuliogopea maisha yetu na ndipo tukafanya jambo hili.


Watakonda kwa njaa, wataangamizwa kwa homa kali. Nitaleta nyama wenye meno makali kuwashambulia, na nyoka wenye sumu wanaotambaa juu ya mavumbi.


Wageni walivunjika moyo; wakakuja kutoka makimbilio yao wakitetemeka.


Yawe akaogopesha falme zote jirani za inchi ya Yuda, zikaogopa kupigana vita na Yosafati.


Wafalme wote wa dunia wamuheshimu, watu wa mataifa yote wamutumikie.


Watakuja makundi kwa makundi na kuyajaza mabonde yenye miinuko, mapango ndani ya mawe, miiba, vichaka vyote na mashamba yote ya kukulishia nyama.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite