Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.

Gade chapit la Kopi




Mika 6:8
66 Referans Kwoze  

Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote, na hivi vyote ni mali yangu. Lakini ninachojali mimi, ni mutu munyenyekevu na mwenye moyo wenye kuvunjika, mutu anayetetemeka anaposikia neno langu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


Mukuwe wenye huruma, kama vile Baba yenu anavyokuwa mwenye huruma.


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Lakini muache haki itiririke kama maji, usawa ukuwe kama muto usiokauka.


Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!


Lakini mutendeane wema ninyi kwa ninyi; musameheane kama Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Yawe wa majeshi, Yawe, ndilo jina lake.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


“Heri wale wanaokuwa wamasikini wa roho, maana Ufalme wa mbinguni ni kwao!


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Siku zote yeye anakopesha kwa moyo safi, na watoto wake ni wenye baraka.


Kule kwa mulima Sinai ulishuka toka mbinguni na kuzungumuza nao. Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli, masharti mazuri na amri.


Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza; yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.


Ni vizuri kwa mutu kungojea kwa utulivu wokovu unaotoka kwa Yawe.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Lakini, kwangu ni vizuri kuwa karibu na Mungu. Wewe Bwana wangu Yawe ndiwe usalama wangu. Nitatangaza mambo yote uliyotenda!


kwa sababu umetubu na kunyenyekea mbele yangu, hata umepasua nguo yako na kulia uliposikia maneno yangu juu ya pahali hapa, na juu ya wakaaji wake, na umejinyenyekeza mbele yangu, nami vilevile nimekusikia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?


Ikiwa kile ninachofanya ndicho nisichotaka, maana yake ninakubali ya kuwa Sheria ni nzuri.


Kwa hiyo kasirani ikakuwa juu yake, juu ya inchi ya Yuda na juu ya Yerusalema. Kisha Hezekia akanyenyekea akaacha kuwa na moyo uliojaa majivuno, yeye na wakaaji wa Yerusalema wakajinyenyekeza; kwa hiyo kasirani ya Yawe haikuwafikia wakati wa utawala wa Hezekia.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Naye hakujinyenyekeza mbele za Yawe, kama vile Manase alivyofanya, lakini yeye aliongeza kutenda makosa zaidi.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


Enoki alikuwa anashirikiana na Mungu. Kisha kuzaa Metusela, Enoki aliishi miaka mia tatu, na kupata wana wengine na wabinti.


wakitambua kwa nini nilipingana nao na kuwapeleka katika inchi ya waadui zao, kama kweli moyo wao mugumu ukinyenyekea na kutubu uovu wao,


Maombi yake na jinsi Mungu alivyomupokea, zambi zake zote na ukosefu wa uaminifu kwake, pahali alipojenga pa kutambikia na jinsi alivyotengeneza sanamu za Ashera na sanamu zingine mbele ya kujinyenyekeza, vimeandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Waonaji.


Wewe muke mwamini unaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa mume wako? Au wewe mume mwamini utaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa muke wako?


Hata hivyo, watu wachache kati ya makabila ya Aseri, Manase na Zebuluni, walijinyenyekeza wakakuja Yerusalema.


Yesu akamujibu: “Ewe bwana, ni nani aliyeniweka kuwa mwamuzi wenu au mutu wa kuwagawanyia mali zenu?”


“Leo hii ninawapa uchaguzi kati ya mema na mabaya, kati ya uzima na kifo.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki, maana ninakaribia kuwaokoa, watu wataona wazi kwamba ninawakomboa.


Tena, nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa naye akiacha zambi yake, akianza kutenda mambo yanayokuwa ya haki na sawa, hatakufa.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoe hukumu kwa haki, mutende mema na kuwa na huruma ninyi kwa ninyi.


Kwa hiyo mutatii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mukifuata amri zake na masharti yake ambayo ninawaamuru leo.”


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Zaburi ya Daudi. Wimbo wangu unaelekea wema na haki; ninauimba kwa heshima yako, ee Yawe.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Aliwapatia haki wamasikini na wakosefu, na mambo yake yaliendeka vizuri. Si hivi ndivyo kunijua mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite