Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.

Gade chapit la Kopi




Mika 6:2
19 Referans Kwoze  

Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Umeiweka dunia imara juu ya misingi yake, isitikisike hata milele.


Yawe alipovikaripia, pumzi ya pua yake ilifunua vilindi vya bahari na misingi ya dunia ikaonekana.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


Yawe anasema hivi: Kama mbingu zinaweza kupimwa, na misingi ya dunia kuchunguzwa, basi, nitawatupilia wazao wa Israeli, kwa sababu ya mambo yote waliyotenda.


Vishindo hivyo vitasikilika mpaka mwisho wa dunia, maana Yawe ana mashitaki juu ya mataifa; anawahukumu wanadamu wote, naye atawaua waovu kwa upanga! –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, mimi nitawashitaki ninyi, na nitawashitaki wazao wenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Munikumbushe tena makosa yangu, tusambe nanyi, mutoe mashitaki yenu kusudi tuuone ukweli wenu!


Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi: Enyi wakaaji wa Yerusalema na watu wa Yuda, tafazali mukuwe waamuzi kati yangu na shamba langu.


wakati alipowekea bahari mupaka wake kusudi maji yake yasipate kuvunja amri yake, wakati alipoweka misingi ya dunia.


Halafu, dunia ikatetemeka na kutikisika, misingi ya mbinguni ikayumbayumba na kuruka, kwa maana Mungu alikuwa amekasirika.


Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake.


Musikilize jinsi Yawe anavyosema: Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima, navyo vilima visikie sauti yako.


Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite