Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.

Gade chapit la Kopi




Mika 6:12
29 Referans Kwoze  

Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.


Nisiwaazibu kwa sababu ya mambo haya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Nisililipize kisasi taifa kama hili?


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Vinywa vyao ni kama kaburi wazi, ndimi zao ni za kudanganya, ndani ya midomo yao munatoka sumu kali sawa ya nyoka.


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Hawasemi vizuri juu ya wengine, wanatunga tu uongo juu ya wanainchi watulivu.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Yuda, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamezarau sheria zangu, wala hawakufuata masharti yangu. Wamepotoshwa na miungu ileile babu zao waliyoifuata.


Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo na kujinyoosha juu ya matandiko yao, mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!


Lakini walimudanganya kwa maneno yao; walimwambia uongo.


Uniokoe, ee Yawe, kutoka watu wadanganyifu na waongo.


Siku hiyo nitawaazibu wote wanaoruka kizingiti cha nyumba kama wapagani, wanaojaza nyumba ya bwana wao vitu vya mateso na udanganyifu.


Wayuda wakamwunga mukono, wakisema kwamba maneno yale yote ni ya kweli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite