Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wakati ule, nitawaondoa farasi wenu, na kuyaharibu magari yenu ya vita. –Ni ujumbe wa Yawe.–

Gade chapit la Kopi




Mika 5:9
15 Referans Kwoze  

Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Mufalme anamutumainia Yawe; kwa wema wa Mungu Mukubwa atakuwa salama.


Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Ee Yawe, simama sasa uwaazibu! Usiwasahau wanaoteswa.


Kwa maana Kristo anapaswa kutawala mpaka atakapowashinda waadui zake wote na kuwaweka chini ya miguu yake.


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Yawe anasema hivi: Sasa mimi nitasimama; sasa nitajiweka tayari; sasa mimi nitatukuzwa.


Nitapigana nawe; nitayeyusha uchafu wako kabisa, na kuondoa takataka yako yote.


Hivyo Mungu akainua mukono, akaapa kwamba atawaangamizia katika jangwa,


na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite