Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Nitakomesha matendo yenu ya uchawi, nanyi hamutakuwa tena na waaguzi.

Gade chapit la Kopi




Mika 5:11
10 Referans Kwoze  

Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Yeye ndiye anayewaangamiza wenye nguvu, na kuziharibu kuta zao zenye nguvu.


Kwa hiyo fujo ya vita itawafikia watu wako, kuta zako zote zitaharibiwa. Kama vile mufalme Salmani alivyoharibu Beti-Arbeli katika vita, wamama wakapondwa pamoja na watoto wao.


Nitakwenda kuishambulia inchi isiyokuwa na kuta, inchi ambako wanainchi wake wanaishi kwa amani. Wote wanakaa katika miji isiyokuwa na kuta; hawana vifungio wala milango.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Inchi yenu imeharibiwa kabisa; miji yenu imeteketezwa kwa moto. Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile Sodoma.


Yawe ameharibu bila huruma makao yote ya wazao wa Yakobo. Kwa kasirani yake amevibomoa vikingio vya watu wa Yuda. Ametupa chini na kuchafua ufalme wao na watawala wake.


Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazao wa Yakobo. Maana kweli wachawi kutoka mashariki wamejaa kati yao; kuna waaguzi kama vile kwa Wafilistini. Wanashirikiana na watu wageni.


Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite