Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku ile, nitawakusanya waliolemewa, nitawakusanya waliopelekwa katika uhamisho, watu wale ambao niliwaazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.–

Gade chapit la Kopi




Mika 4:6
16 Referans Kwoze  

Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


–Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe, yule anayewakusanya Waisraeli waliosambazwa.– Zaidi ya hao niliokwisha kukusanya, nitawakusanya watu wengine wakutane nao.


Yawe anajenga tena Yerusalema; anawarudisha Waisraeli waliopelekwa katika uhamisho.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


Nitawaondoa ninyi katika kila taifa na kuwakusanya kutoka inchi zote za kigeni; nitawarudisha katika inchi yenu wenyewe.


Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini, nitawakusanya kutoka miisho ya dunia. Wote watakuwa pale; hata vipofu na vilema, wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa; kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.


Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.


Ninakuomba tu waadui wasinisimange, wasijitukuze juu ya kuanguka kwangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite