Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 4:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia. Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe, nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!

Gade chapit la Kopi




Mika 4:11
15 Referans Kwoze  

Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Ikakuwa katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, mwaka wa kenda wa utawala wa Zedekia, Nebukadneza mufalme wa Babeli, alifika na waaskari wake wote kuushambulia Yerusalema, wakauzunguka kila upande.


Wafezeheke na kurudishwa nyuma, wote wale wanaouchukia Sayuni.


Lakini Asuria hakuwazia hivyo, yeye alikuwa na nia ingine; alikusudia kuharibu kabisa, kuangamiza mataifa mengi sana.


Aha! Ngurumo ya watu wengi! Wananguruma kama bahari. Aha! Mulio wa watu wa mataifa! Yanatoa mulio kama wa maji mengi.


Halafu, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema, wote wanaoshambulia ukuta wake na kuutia wasiwasi, watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitapingana nawe ewe Tiro. Nitasukuma mataifa mengi juu yako, nao watakuja kama mawimbi ya bahari.


Wanasema: “Mukuje tuangamize taifa lao, hata jina la Israeli lisikumbukwe tena.”


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe ndiwe niliyesema habari zako hapo zamani kwa njia ya watumishi wangu manabii wa Israeli, ambao walitabiri nyakati zile kwamba nitakuleta kusudi ushambulie watu wa Israeli.


Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite