Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.

Gade chapit la Kopi




Mika 4:10
27 Referans Kwoze  

Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia. Lakini yeye ni mutoto mupumbafu; wakati wa kuzaliwa unapofika yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!


Nitaiharibu mizabibu yake na tini zake, anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake. Nitaifanya ikuwe pori, nao nyama wa pori wataikula.


Ni mimi niliyemwamuru Kiro akuje, atimize mapenzi yangu. Nitazifanikisha njia zake zote. Ataujenga upya muji wangu Yerusalema, na kuwapa uhuru watu wangu wanaokuwa katika uhamisho, bila kutaka malipo wala zawadi. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yawe, Mukombozi wenu, Mutakatifu wa Israeli, anasema hivi: Kwa ajili yenu nitatuma waaskari kwenda Babeli. Nitavunja vifungio vya milango ya muji wake, na kelele za wale Wakaldea zitageuka maombolezo.


Tena wamoja kati ya watoto wako wanaume watapelekwa, nao watakuwa matowashi katika nyumba ya mufalme wa Babeli.”


Lakini yule mwanamuke akapewa mabawa mawili yanayokuwa kama ya tai, kusudi apate kuruka kwenda katika jangwa kwenye nafasi aliyotengenezewa, mbali na yule nyoka. Na kule apate kukulishwa kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Nitakuokoa toka katika mikono ya watu waovu, na kukuopoa toka katika makucha ya watesaji.


Aliwaokoa katika mikono ya waliowachukia; aliwaokoa kutoka nguvu za waadui zao.


Watu waliookolewa kwenye vita aliwapeleka katika uhamisho Babeli. Kule wakakuwa watumwa wake na wa wazao wake mpaka ufalme wa Persia ulipoinuka kwa nguvu.


Kwa hiyo, Yawe akawaleta majemadari wa jeshi la mufalme wa Asuria. Hao majemadari wakamukamata Manase kwa ndoana, wakamufunga kikomo cha shaba, wakamupeleka mpaka Babeli.


Basi, sehemu ya ukuta wa muji ukabomolewa, naye mufalme pamoja na waaskari wote wakakimbia wakati wa usiku wakipitia katika bustani ya mufalme kwenye mulango katikati ya kuta mbili, wakaenda upande wa Araba, ingawa Wababeli walikuwa wameuzunguka muji.


Enyi wote niliowaondoa kutoka Yerusalema na kuwapeleka katika uhamisho kule Babeli, musikilize neno langu mimi Yawe.


Miji yake itatekwa, kuta zake vilevile. Siku hiyo mioyo ya waaskari wa Moabu itakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Mufalme Nebukadneza wa Babeli aliwapiga na kuwaua watu hao kule Ribla katika inchi ya Hamati. Basi, hivi ndivyo watu wa Yuda walikwenda katika uhamisho inje ya inchi yao.


Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.


“Hivi ndivyo anavyosema Kiro mufalme wa Persia: ‘Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote za ulimwengu, na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, katika inchi ya Yuda. Basi sasa kila mutu kati yenu, ninyi wote munaokuwa watu wa Yawe, Mungu wake akuwe pamoja naye, na aende.’ ”


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Twaa ule mukaba ulioununua na ambao unaouvaa katika kiuno, uende kwenye muto Furati na kuuficha katika pango chini ya jiwe.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite