Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.

Gade chapit la Kopi




Mika 3:9
16 Referans Kwoze  

Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


wamenenepa na kungaa vizuri. Maovu yao hayana mwisho, hawahukumu yatima kwa kufuatana na sheria kusudi wapate kufanikiwa, wala hawatetei haki za watu wakosefu.


kama mukizarau masharti yangu na kuchukia kwa roho maagizo yangu mukiacha kutii amri zangu zote na kuvunja agano langu,


Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!


Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki.


Ukali wa waovu utawaangamiza, maana wanakataa kutenda mambo ya haki.


Makuhani watafundisha taifa langu kupambanua vitu vinavyokuwa vitakatifu na visivyokuwa vitakatifu, na kuwajulisha tofauti kati ya vitu vinavyokuwa vichafu na visivyokuwa vichafu.


Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.


Nikawakaripia viongozi wa watu wa Yuda, nikisema: “Uovu gani huu munaofanya, kuichafua siku ya Sabato?


Mutu mubaya anapokea kituliro kwa siri kusudi apate kupotosha haki.


Angalisho, enyi munaogeuza sheria kuwa uchungu, na kuona haki kuwa kama takataka!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite