Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.

Gade chapit la Kopi




Mika 3:8
28 Referans Kwoze  

Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Mafundisho yangu na mahubiri yangu hayakutolewa kwa maneno ya werevu na hekima ya kimutu, lakini katika onyesho la uwezo wa Roho wa Mungu,


Sasa, ewe mwanadamu, uwaelezee Waisraeli habari za nyumba ya Mungu na wajifunze taswira yake. Wapate haya kutokana na machukizo yao waliyotenda.


Wewe mwanadamu, ujulishe Yerusalema machukizo yake.


Niko na maneno mengi sana, roho yangu inanisukuma kusema.


kwa maana hakuwafundisha sawa vile walimu wao wa Sheria, lakini kama vile mutu mwenye mamlaka.


Ewe mwanadamu! Uko tayari kutoa hukumu, kuuhukumu muji huu wa wauaji? Basi, ujulishe machukizo yake yote.


Wewe mwanadamu, uko tayari kuwahukumu watu hawa? Basi, uwahukumu. Uwajulishe mambo wazee wao waliyofanya.


Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Na tangu leo, ninakufanya kuwa imara kama muji unaozungukwa na kuta, kama munara wa chuma na kama ukuta mugumu sana wa shaba. Utakuwa na nguvu juu ya inchi yote, juu ya wafalme wa Yuda, wakubwa wake, makuhani wake na watu wake wote.


Nimejaa hasira ya Yawe nami ninachoka kwa kuizuia. Kwa hiyo Yawe akaniambia: Umwange hasira ile katika barabara juu ya watoto na vilevile juu ya makundi ya vijana; nayo itawaangukia wote, mume na muke, nao wazee na hata wale ambao wamezeeka sana.


Yakobo na ndugu yake Yoane, wote wawili walikuwa wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa jina la Boanerge, maana yake ngurumo ya radi),


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu. Hawakufichua wazi uovu wako kusudi wapate kukurudishia hali yako ya mbele. Lakini walikuonea maono ya uongo na ya kupotosha.


Yawe aliniambia: Wewe mwanadamu! Uko tayari kuwahukumu Ohola na Oholiba? Basi, uwatangazie matendo yao ya kuchukiza!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite