Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo, watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema: Tumeangamia kabisa; amekamata inchi yetu, ameiondoa katika mikono yetu. Mashamba yetu ameyagawanya kwa wale waliotuteka.

Gade chapit la Kopi




Mika 2:4
35 Referans Kwoze  

Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo na kumutungia misemo ya kitambi: Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako, na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi! Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?


Enyi wakaaji wa Maresa, Mungu atawaletea tena adui atakayewateka. Waongozi waheshimiwa wa Israeli watakimbilia ndani ya pango kule Adulamu.


Yawe anasema: Nitaifanya Yerusalema kuwa mabomoko matupu, nitaifanya kuwa pango la mbweha; na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa, pahali pasipokaliwa na mutu yeyote.


Dunia itaharibiwa kabisa na kuangamizwa. Ni Yawe amesema hayo.


Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.


Mutakwenda kwa kupapasapapasa muchana kama vipofu wala hamutafanikiwa katika shuguli zenu. Mutakuwa munateswa kila mara na hakutakuwa mutu wa kuwasaidia.


Balamu akamutolea Balaki mashairi yake, akasema: Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, hakika, mufalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki: Kuja uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, hakika, kuja uwakaripie Waisraeli!


Basi hao wakubwa wakatafuta kumukamata Yesu, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao. Lakini kwa sababu waliogopa kundi la watu, wakamwacha ajiendee.


Nitateketeza kabisa viumbe vyote katika dunia:


Musimame! Muende! Hapa hakuna tena pahali pa kupumzika! Kwa ajili ya ukosefu wenu wa uaminifu, maangamizi makubwa yanawangojea!


Kutakuwa kilio katika mashamba yote ya mizabibu; maana nitapita kati yenu kwa kuwaazibu. Ni Yawe anayesema hivyo.


Musikilize maombolezo yangu juu yenu, enyi Waisraeli:


Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.


Mulie kama vile binti aliyevaa gunia akiombolezea kifo cha muchumba wake.


Ewe Yerusalema! Mutu akitaka kutumia mezali juu yako atasema hivi: Kama vile mama anavyokuwa ndivyo binti wake anavyokuwa.


Basi akakikunjua mbele yangu, nacho kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma maneno ya maombolezo, kilio na hasara.


Nikienda inje katika mbuga, ninaiona maiti ya waliouawa kwa vita; nikiingia ndani katika muji, ninaona tu maiti ya waliokufa kwa njaa! Manabii na makuhani wanashugulikia mambo yao katika inchi, lakini hawajui wanalofanya.


Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!


utaimba wimbo huu wa kumuchekelea mufalme wa Babeli: Jinsi gani mutesaji alikomeshwa! Ukali wake umekomeshwa!


Yobu akaendelea kutoa masemi yake, akasema:


Nabii Yeremia vilevile akatunga shairi la maombolezo kwa ajili ya kifo chake; nao waimbaji wote, wanaume na wanawake, wanamutaja Yosia katika maombolezo yao, mpaka leo. Wakakusudia kuwa wanafanya maombolezo haya katika Israeli; angalia nayo yameandikwa katika Maombolezo.


Daudi aliimba maombolezo haya kwa ajili ya Saulo na mwana wake Yonatani.


Basi, Balamu akasema mashairi haya: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Beori, mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho,


naye akasema mashairi haya ya Yawe: Mashairi yangu mimi Balamu mwana wa Peori mashairi ya mutu aliyefumbuliwa macho.


Halafu, Balamu akamutolea Balaki mashairi yake: Simama, Balaki, usikie! Unisikilize, ewe mwana wa Sipori!


Nyumba zao zitapewa watu wengine, nayo mashamba yao na wake zao vilevile; maana nitaunyoosha mukono wangu, kuwaazibu wakaaji wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, wake zao nitawatoa kwa waume wengine, nayo mashamba yao nitawapa wengine. Maana, tangu mudogo mpaka mukubwa, kila mumoja ana tamaa ya faida isiyokuwa ya haki. Tangu manabii mpaka makuhani, kila mumoja anatenda kwa udanganyifu.


Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza; nitatembea uchi na bila viatu. Nitaomboleza na kulia kama mbweha, nitasikitika na kulia kama mbuni.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri na kuwaita wanawake waombolezaji; muwaite wanawake wanaoelewa nyimbo za kilio.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite