Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninapanga kuwaletea ninyi hasara, ambayo hamutaweza kuiponyoka hata kidogo. Utakuwa wakati mubaya kwenu, wala hamutaweza kutembea kwa maringo.

Gade chapit la Kopi




Mika 2:3
29 Referans Kwoze  

Basi, kutakuwa wakati mubaya ambao hata mwenye hekima atanyamaza.


Watu wote watakaobaki wa jamaa hii mbaya, pahali popote pale nilipowasambaza, wataona heri kufa kuliko kuishi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Basi Sasa, uende kuwaambia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema kwamba: Yawe anasema hivi: Mimi nimekwisha kukamata mipango juu yenu, na nimekusudia kuleta hasara juu yenu. Basi kila mumoja arudi kutoka katika njia mbaya, abadilishe mwenendo wake na matendo yake.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Tunalazimishwa kufanya kazi kama punda, tumechoka, lakini haturuhusiwi kupumzika.


Yawe amefanya yale aliyokusudia, ametimiza yale aliyoagiza. Kama alivyopanga tangu kale, ameangamiza bila huruma yoyote. Amewafanya waadui wafurahie azabu yako, amewatukuza mashujaa wa waadui zako.


Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.


Wao walijitolea kufa kwa kuokoa maisha yangu. Ninawashukuru, wala si mimi peke yangu tu, nayo makanisa yote ya inchi za watu wa mataifa wanawashukuru vilevile.


Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.


Hata wale wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kutoroka; wenye nguvu wataishiwa nguvu zao, na waaskari watashindwa kuyaokoa maisha yao.


Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.


Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.


Yehudi alipokuwa amekwisha kusoma vipindi vitatu au vine hivi vya kitabu kile, mufalme alivikatakata kwa kisu na kuvitupa katika moto wa makaa. Aliendelea kufanya hivyo mpaka kitabu chote kikateketezwa.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Yeremia akamwambia Zedekia mufalme wa Yuda, mambo hayohayo, akisema: Mukubali kubeba nira mufalme wa Babeli atakayowalazimisha kubeba. Mumutumikie yeye na watu wake, kusudi mupate kuishi.


Wanasema: Muache Yawe afanye haraka, tunataka kuona yale aliyosema atayafanya! Mutakatifu wa Israeli atimize basi kusudi lake kusudi tuone ana mipango gani!


Yawe anasema: Wanawake wa Sayuni wako na kiburi; wanatembea wakiinua kichwa juu, wakirembua macho yao kwa tamaa. Hatua zao ni za maringo, nao wanalilisha mikufu kwenye miguu yao.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite