Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.

Gade chapit la Kopi




Mika 2:12
28 Referans Kwoze  

Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waisraeli wataniomba niwafanye kuwa wengi kama kundi la kondoo, nami nitawafanya hivyo.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.


Basi, nitashusha moto juu ya muji wa Temani, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Bosira.


uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika inchi yao.


Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Lakini mimi nitawaokoa kondoo wangu wasiendelee tena kuteswa. Nitatoa hukumu juu ya kila kondoo.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.


Kisha, nitawakusanya kondoo wangu waliobaki kutoka inchi zote nilipowafukuza, na kuwarudisha katika malisho yao. Nao watazaa na kuongezeka.


Upanga utajaa damu na mafuta: damu ya kondoo na mbuzi, na mafuta ya figo za kondoo dume. Maana Yawe ana sadaka huko Bosira, kutakuwa mauaji makubwa katika inchi ya Edomu.


Siku hiyo, Yawe atapepeta ngano yake kutokea kwenye muto Furati mpaka kwenye mupaka wa Misri, nanyi Waisraeli mutakusanywa mumojamumoja.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.


Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosira akatawala pahali pake.


Wana-kondoo watakula majani kule, kama vile katika shamba la kuwakulishia. Wana-mbuzi wanono watatafuta chakula chao kule kule.


Yule atakayepasua njia atawatangulia, nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje, mutapita na kutoka inje. Mufalme wenu, atawatangulia; Yawe mwenyewe atawatangulia.


Nawe kilima cha Yerusalema, wewe munara wa Sayuni, ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake, kama muchungaji juu ya kondoo wake, wewe utakuwa tena muji wenye mamlaka sawa zamani. Yerusalema utakuwa tena muji mukubwa wa mufalme.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Nitawatoa kutoka kwa watu wa mataifa. Nitawakusanya kutoka inchi za mbali na kuwaleta katika inchi yao wenyewe. Nitawachunga juu ya milima ya inchi ya Israeli, kandokando ya vijito na katika sehemu zote za inchi zinazokaliwa na watu.


Wakati huo nitawakusanya, na kuwafanya mujulikane na kusifiwa kati ya watu wote katika dunia, na kuwarudishia hali yenu njema, nanyi mutaona kwa macho yenu wenyewe. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite