Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.

Gade chapit la Kopi




Mika 2:1
40 Referans Kwoze  

Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema.


Matendo ya watu wadanganyifu ni mabaya; hao wanatunga maneno mabaya kwa kumwangamiza masikini kwa maneno ya uongo, hata kama masikini ni mwenye sheria.


Ndani yako kumetoka mumoja aliyepanga maovu juu ya Yawe. Huyu mutu anafanya shauri baya sana.


wasingiziaji, wenye kumuchukia Mungu, wenye kasirani, wenye kiburi na wenye kujivuna. Wao ni werevu kwa kutenda mabaya, hawatii wazazi wao,


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Maana mikono yenu imechafuka kwa damu, na vidole vyenu kwa matendo maovu. Midomo yenu imesema uongo, na ndimi zenu zinasema uovu.


Waovu hawalali hata kidogo wasipotenda uovu; hawapati usingizi wasipomukwaza mutu.


Usimunyime mutu anayehitaji musaada, ikiwa una uwezo wa kufanya hivyo.


Nina uwezo wa kukuzuru; lakini Mungu wa baba yako alinitokea usiku wa kuamukia leo, akaniambia nifanye angalisho, akisema: ‘Ujichunge! Usimwambie Yakobo neno lolote, zuri au baya’.


Kesho yake kulipokucha, Wayuda wakafanya shauri; wakafanya kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo kwanza.


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Watoto wenu wanaume na wanawake watatolewa kwa watu wengine nanyi mutakodoa macho muchana kutwa kuwatazamia warudi, lakini hamutakuwa na nguvu ya kufanya chochote.


Basi sasa, ninyi pamoja na Baraza Kubwa mumwombe jemadari awaletee Paulo, mukimwambia tu kwamba munataka kuchunguza vizuri zaidi maneno yake. Na sisi tuko tayari kumwua mbele hajafika hapa.”


Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.


Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu, hawa ndio watu wanaofanya mipango ya uovu na kutoa mashauri mabaya katika muji huu.


Lakini Esteri alipomwendea mufalme, naye mufalme akatoa amri kwa waandishi kwamba lile shauri baya ambalo Hamani alikuwa amefanya juu ya Wayuda, limurudilie yeye mwenyewe; na ya kuwa yeye na wana wake wauawe kwa kutundikwa kwenye muti.


Basi, muke wake Zeresi na warafiki zake wakamushauria hivi: “Kwa nini asitengenezewe muti wa kutundikia, wenye urefu wa metre makumi mbili na mbili? Kesho asubui, unaweza kuzungumuza na mufalme kusudi Mordekayi auawe juu yake, kisha uende ukule karamu na mufalme kwa furaha.” Wazo hilo lilimufurahisha Hamani, naye akatengeneza muti ule.


Basi, Hamani akamwambia mufalme: “Kuna watu wa taifa moja wanaokuwa kila nafasi katika utawala wako, nao wako katika kila jimbo. Watu hao wana sheria zinazokuwa tofauti kabisa na za watu wengine. Vilevile, wao hawazitii sheria zako, kwa hiyo haikufaidii kwa kitu chochote kuwavumilia.


Mwuaji anaamuka asubui mapema, kwa kwenda kuwaua wamasikini na wakosefu, na usiku ukifika, kazi yake ni kuiba.


Anayepanga kutenda maovu kweli anakosa! Wanaopanga kutenda mazuri watapata mema na uaminifu.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Munategemea silaha zenu, munafanya mambo ya kuchukiza na kila mwanaume kati yenu analala na muke wa jirani yake! Munazani kwamba mutapewa inchi hii ikuwe yenu?


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile, utaanza kuwaza ndani ya moyo wako na kupanga mipango miovu na kusema:


Mufalme hapaswi kunyanganya hata kidogo mali ya watu. Sehemu ya inchi yoyote anayowapa watoto wake wa kiume inapaswa kutokana na eneo lake mwenyewe. Hivyo hatawatesa watu wangu kwa kuwanyanganya urizi wao.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Musiwatese wajane, wayatima, wageni au wamasikini; musipange kutendeana mabaya ndani ya mioyo yenu.


Hapo, Yezebeli, muke wake, akamwambia: “Anayetawala Israeli ni nani? Si ni wewe? Amuka, ukule na uchangamuke. Mimi peke yangu nitakupa shamba la mizabibu la Naboti wa Yezereheli.”


Wanatunga udanganyifu na kuzaa uovu. Mioyo yao inapanga udanganyifu.


Anapolala anawaza kutenda maovu, anajiweka katika njia isiyokuwa nzuri, wala hachukii uovu.


Hapana. Ninyi munafikiria tu kutenda maovu; ninyi wenyewe munaeneza mateso makali katika inchi.


Yawe anawashitaki wazee na wakubwa wa watu wake: Ninyi ndio mulioliharibu shamba la mizabibu; mali wamasikini walizonyanganywa ziko ndani ya nyumba zenu.


Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite