Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mika 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.

Gade chapit la Kopi




Mika 1:4
12 Referans Kwoze  

Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Milima inayeyuka kama inta mbele ya Yawe, mbele ya Bwana wa dunia yote.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Akisimama dunia inatikisika; akiyatupia mataifa jicho, hayo yanatetemeka. Milima ya milele inavunjwavunjwa, vilima vya zamani za kale vinaanguka; ni juu yao kulipokuwa njia zake za kale na kale.


Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.


Ee Yawe, ulipotoka kule Seiri, ulipoteremuka kwenye mulima Edomu, inchi ilitetemeka, mbingu zilidondosha maji, mawingu yakaiangusha mvua.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.


Mungu asimame sasa, na waadui zake watawanyike! Wanaomuchukia wakimbie mbali naye!


Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite