Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Chagua mafundisho yangu pahali pa feza; na maarifa pahali pa zahabu safi.

Gade chapit la Kopi




Mezali 8:10
15 Referans Kwoze  

Kweli, ninapenda amri zako, kuliko hata zahabu safi kabisa.


Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Hekima ni ya bei kubwa kama urizi; ni ya mafaa kwa wale wote wanaokuwa wazima.


Maneno ya mwenye haki ni kama feza bora. Akili ya mutu mwovu haifai kwa kitu chochote.


Lakini Petro akamwambia: “Sina mali yoyote, lakini nitakupa kile ninachokuwa nacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ninakuamuru simama utembee!”


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Ninafurahi kwa sababu ya neno lako, kama mutu aliyekuta kitu cha bei kali.


tunahuzunishwa lakini tunafurahi siku zote. Tunaonekana kama wamasikini lakini tunatajirisha watu wengi, hatuna kitu, lakini tunakuwa na vitu vyote.


Matunda yangu ni mazuri kuliko zahabu safi, na faida yangu inashinda ya feza bora.


Hekima haiwezi kupatikana kwa zahabu, wala kwa kupima kiasi kingi cha feza.


Zahabu au kioo havilingani nayo, wala haiwezi kubadilishwa na mawe ya zahabu safi.


Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite