Naye kuhani wa hekalu la mungu Zeu, lililokuwa kwenye kiingilio cha muji, akaleta ngombe waliopambwa na mafungu za maua mbele ya mulango. Maana yeye pamoja na kundi la watu walitaka kuwatolea wale mitume sadaka ya nyama wenye kuchinjwa.
Basi, Pashuri akamupiga nabii Yeremia na kumutia katika minyororo iliyokuwa upande wa mulango wa juu wa kuingilia katika nyumba ya Yawe, ulioitwa mulango wa Benjamina.
Hakutambua kwamba maisha yake yako katika hatari, mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mushale ndani ya moyo, amekuwa kama ndege aliyerukia ndani ya wavu.