2 Kwa hiyo, utaweza kulinda akili, na kinywa chako kitashika maarifa.
Moyo wa mwenye hekima unamwezesha kusema kwa hekima; unayafanya maneno yake yakuwe ya kuvutia.
Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.
Midomo yako inadondosha asali, ee muchumba wangu, ulimi wako una asali na maziwa. Harufu nzuri ya nguo zako ni kama miti ya Lebanoni.
Ulimi wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini watu wapumbafu wanamwanga maneno ya ujinga.
Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.
Nitarudiliarudilia kwa sauti maamuzi yako yote uliyotoa.
Kinywa changu kitaeleza matendo yako ya haki, nitatangaza muchana kutwa matendo yako ya wokovu ijapokuwa hayo yanapita akili yangu.
Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.
Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!
Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako,