Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 5:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?

Gade chapit la Kopi




Mezali 5:12
23 Referans Kwoze  

Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.


Mupumbafu anazarau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ni mwenye akili.


mumetupilia mashauri yangu yote, mumezarau maonyo yangu.


“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?


Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa, lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho.


Hata hivyo, mimi niliwatuma kwenu siku zote watumishi wangu manabii nikisema: Musifanye jambo hili baya ninalolichukia!


Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


nilikuwa mupumbafu na mujinga, nilikuwa kama nyama mbele yako.


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Lakini wao wakasema: “Utupitishe! Wewe ulikuja huku ukiwa mugeni na sasa unajifanya kuwa mwamuzi! Basi, tutakutendea mabaya zaidi ya wale wageni wako.” Halafu wakamusukuma Loti nyuma hata karibu wavunje mulango wake.


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


Kwa mwisho wa maisha yako utaomboleza, wakati mwili wako utakapoangamizwa.


Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”


Anayekubali kufundishwa anaelekea kwenye uzima, lakini anayekataa kuonywa amepotoka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite