Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Jambo la musingi ni kujipatia hekima; toa vyote unavyokuwa navyo ujipatie akili.

Gade chapit la Kopi




Mezali 4:7
18 Referans Kwoze  

Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Kwa kanuni zako ninapata hekima, kwa hiyo ninachukia kila mwenendo mubaya.


Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”


Mali inayopatikana kwa udanganyifu ni muvuke unaopita na mutego wa kifo.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Ujipatie hekima, ujipatie ufahamu; usisahau wala kuzarau maneno yangu.


Nilifanywa kwa mwanzo wa nyakati, nilikuwa niko mbele ya dunia kuanza.


Kwa hiyo, ninakuomba unipe hekima na maarifa kusudi niweze kuwatawala watu wako vizuri. Kama sivyo, nitaweza namna gani kuwatawala hawa watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


ukitafuta hekima kama feza, na kuitaka kama hazina iliyofichwa,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite