5 Ujipatie hekima, ujipatie ufahamu; usisahau wala kuzarau maneno yangu.
Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.
Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata njia za Daudi babu yake, na kushika amri za Yawe kwa uangalifu.
Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.
Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?
Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.
Hayo yote yametupata sisi ijapokuwa hatujakusahau, wala hatujavunja agano lako.
Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.
Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.
Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.
Waadui na watesaji wangu ni wengi, lakini mimi sigeuki mbali na maagizo yako.
Wasiomujali Mungu wananizarau siku zote, lakini mimi sigeuki mbali na sheria yako.
Ninamufuata kabisa; njia yake nimeishikilia wala sikugeuka pembeni.
Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu.
Jambo la musingi ni kujipatia hekima; toa vyote unavyokuwa navyo ujipatie akili.