Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene, hawajui kinachowafanya wajikwae.

Gade chapit la Kopi




Mezali 4:19
16 Referans Kwoze  

Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


Kwa hiyo njia zao zitakuwa zenye utelezi na giza, watajigonga na kuanguka; maana, nitaleta hasara juu yao mwaka wa kuwaazibu utakapotimia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Lakini kama mutu akitembea usiku, anajikwaa, kwa sababu hana mwangaza ndani yake.”


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Halafu mimi nitawaambia hivi waziwazi: ‘Sikuwajua ninyi hata siku moja. Mutoke karibu nami, ninyi watenda maovu.’


watu wanaoacha njia zenye kunyooka kwa kufuata njia za giza,


Ameondolewa toka katika mwangaza, akatupwa katika giza; amefukuzwa mbali kutoka katika dunia.


wakipapasapapasa katika giza kusikokuwa mwangaza; na kuwafanya wapepesuke kama walevi.


Wao wanapatwa na giza wakati wa muchana; muchana kati wanapapasapapasa kama vile usiku.


Lakini anayemuchukia ndugu yake anaishi na kutembea katika giza, wala hajui pahali anapokwenda kwa sababu giza limemupofusha macho.


“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!


Njia ya waovu imejaa miiba na mitego; anayetaka kulinda maisha yake ataiepuka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite