14 Usijiingize katika njia ya waovu, wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.
Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;
Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”
Wewe mwana wangu usiandamane nao, uzuie muguu wako usifuatane nao.
Mwana wangu, usikubali kushawishiwa na wenye zambi.
Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.
Achana na ujinga upate kuishi; fuata njia ya akili.”
Epuka njia hiyo wala usiikaribie; ujiepushe nayo, uende zako.
Uepushe njia yako mbali naye, wala usiukaribie mulango wa nyumba yake,
Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile, karibu na pahali mwanamuke mumoja alipoishi. Basi akashika njia inayokwenda kwa mwanamuke yule.
Usijifunze mwenendo wake, na kujinasa kabisa katika mutego.
Usiwaonee wivu watu waovu, wala usitamani kuwa pamoja nao,