Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 4:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.

Gade chapit la Kopi




Mezali 4:13
20 Referans Kwoze  

Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.


Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.


Nunua ukweli, wala usiuuzishe; nunua hekima, mafundisho na akili.


Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Simoni Petro akamujibu: “Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unasema maneno ya uzima wa milele.


Wandugu zetu wamemushinda kwa nguvu ya damu ya Mwana-Kondoo na kwa njia ya ukweli walioshuhudia. Wao walikubali kutoa maisha yao mpaka kufa.


Ninajua pahali pale unapokaa, ile ndiyo nafasi ya utawala wa Shetani. Wewe unashikamana na jina langu, wala haukuikana imani unayokuwa nayo kwangu, hata wakati Antipa, mushuhuda wangu mwaminifu, alipouawa kati yenu kule kwenye makao ya Shetani.


Mara tu nilipoachana nao, nikamwona mupenzi wangu wa moyo. Nikamushika wala sikumwacha aondoke, mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu, mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.


Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.


navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako, na pambo zuri katika shingo lako.


Mutu yule alipoona kwamba hawezi kumushinda Yakobo, alimugusa Yakobo kwenye maunganio ya kiuno, naye akateguka alipokuwa anapigana naye.


Roho ndiye anayeleta uzima; mwili hauwezi kufaa kitu. Maneno haya niliyosema nanyi, ndiyo Roho na uzima.


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.


Anayekubali kufundishwa anaelekea kwenye uzima, lakini anayekataa kuonywa amepotoka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite