1 Wana wangu, musikilize maadibisho ya baba yenu, mutege sikio mupate kuwa na akili.
Kwa sababu hiyo, tunapaswa kushikamana zaidi na habari tuliyosikia, kusudi tusipotee mbali.
Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.
Mwana wangu, sikiliza mafundisho ya baba yako, wala usizarau mashauri ya mama yako;
Tega sikio usikie maneno ya wenye hekima; elekeza moyo wako kwa maarifa yangu.
Mwana wangu, sikia hekima yangu, tega sikio usikie elimu yangu.
Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.
Uambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”, na Akili: “Wewe ni rafiki yangu”.
Zitawawezesha watu kujua hekima na mafundisho, na kufahamu misemo yenye maana kubwa.
Sisi tumeitii amri hiyo ya babu yetu Yonadabu mwana wa Rekabu siku zote, juu ya jambo alilotuamuru. Sisi hatukunywi divai hata kidogo; sisi wenyewe hatukunywi, wala wake zetu, wala watoto wetu wanaume au wanawake.
“Mukusanyike musikie, enyi wana wa Yakobo, munisikilize mimi Israeli, baba yenu.
Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.