Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.

Gade chapit la Kopi




Mezali 3:9
30 Referans Kwoze  

Kila siku ya kwanza ya juma, kila mumoja wenu anapaswa kuweka akiba ya mali kwake, kwa kadiri ya mapato yake, kusudi musihitaji kufanya muchango wakati nitakapokuja.


Mazao ya kwanza ya shamba lako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Anayemutesa muzaifu anamutukana Muumba wake, lakini anayemwonea huruma mukosefu anamutukuza Mungu.


Mutafanya vile vile juu ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mutamwacha kila muzaliwa wa kwanza na mama yake kwa siku saba na siku ya nane mutanitolea.


Mazao ya kwanza ya shamba yako utayaleta katika nyumba yangu mimi Yawe, Mungu wako. Usipike mwana-kondoo au mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.


Nalo jiwe hili nililosimika hapa kama nguzo, litakuwa nyumba yako Mungu, nami nitakupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”


Kila kazi aliyoifanya katika utumishi wa nyumba ya Mungu au katika kutii sheria na amri za Mungu kwa kufuata uongozi kutoka kwake, alizifanya kwa moyo wake wote, naye akafanikiwa.


Gala zetu zijae mavuno ya kila aina. Kondoo wetu katika mbuga wazae maelfu na maelfu.


Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.


Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.


Mutafanya sikukuu ya mavuno ya kwanza ya kazi zenu na ya mavuno ya mashamba yenu. Mutafanya sikukuu ya kukusanya mavuno mwisho wa mwaka munapokusanya mazao ya kazi zenu.


Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mutakapopika mukate, mukate wa kwanza wa mazao ya kwanza ya ngano yenu utatolewa kama sadaka kutoka pahali pa kupepetea ngano.


Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.


Azaria, Kuhani Mukubwa aliyekuwa wa uzao wa Sadoki akamujibu: “Tangu wakati watu walipoanza kuleta matoleo yao katika hekalu, tumekuwa na vyakula vya kutosha na hata tuna akiba kubwa. Yawe amewabariki watu wake, ndiyo maana tumepata vitu hivi vyote.”


Na yule aliyepata furushi mbili akafaidia zingine mbili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite