Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Umutumainie Yawe kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe.

Gade chapit la Kopi




Mezali 3:5
24 Referans Kwoze  

Umutolee Yawe maisha yako, umutumainie yeye, naye atakufanyia kitu.


Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Wokovu na utukufu wangu vinatoka kwa Mungu; kikingio changu chenye nguvu na kimbilio langu ni Mungu.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.


Ninajua, ee Yawe, mwanadamu hana uwezo juu ya maisha yake; hakuna mutu anayeweza kuongoza maisha yake.


Mukuwe na masikilizano kati yenu. Musikuwe na nia ya kujitukuza, lakini mukubali kuishi katika unyenyekevu. Musijiwazie kuwa wenye akili sana.


Wimbo wa safari za kidini. Wanaomutegemea Yawe, wako kama mulima Sayuni, ambao hautikisiki lakini unabaki imara siku zote.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ninayependa kumufundisha leo ni wewe, kusudi tumaini lako likuwe kwa Yawe.


Mungu aniue akitaka; sina la kupoteza. Hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.


Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.


Kwa hiyo sisi tuliotangulia kumutumainia Kristo, tumusifu Mungu kwa ajili ya utukufu wake!


Wakati mwingine wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku chache tu. Kwa agizo la Yawe, Waisraeli walipiga kambi na ni kwa agizo la Yawe walisafiri.


Ikiwa ni siku mbili, mwezi, mwaka au zaidi, muda wote wingu hilo lilipokuwa juu ya hema, Waisraeli hawakuhama; lakini lilipoinuliwa, nao vilevile walihama.


Kwa hiyo tukafunga na kumwomba Mungu atulinde, naye akayasikia maombi yetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite