26 maana Yawe ndiye atakayekutegemeza, atakuepusha usipate kunaswa katika mutego.
Anayemwogopa Yawe ana tumaini imara, na watoto wake watapata kimbilio salama.
Hakika Mungu atakuokoa katika mutego, atakukinga na magonjwa mabaya.
Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.
Kumwogopa Mungu si ndilo tegemeo lako? Na ukamilifu wa mwenendo wako si ndilo tumaini lako?
Hatakuacha uanguke; mulinzi wako hasinzii.