22 navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako, na pambo zuri katika shingo lako.
Maana hayo ni uzima kwa mutu anayeyapata, ni dawa kwa mwili wake wote.
hayo yatakupamba kilemba cha neema juu ya kichwa chako, kama mukufu katika shingo yako.
Ee Bwana, sisi tunaishi kutokana na yote uliyotenda, kwa hayo yote mimi peke yangu vilevile ninaishi. Unirudishie afya, uniwezeshe kuishi.
Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”
Shika mafundisho ya hekima na usimwache iponyoke, uishike kwa uangalifu maana ni uzima wako.
Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.
Hekima ni chemichemi ya uzima kwa yule anayekuwa nayo, lakini upumbafu ni azabu ya wapumbafu.
Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.
Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.