Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 3:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mwana wangu, shika hekima safi na akili; usiviache vitoweke mbele ya macho yako,

Gade chapit la Kopi




Mezali 3:21
18 Referans Kwoze  

Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.


Usiyaache yatoweke mbele ya macho, uyafunge ndani ya moyo wako.


“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu


Lakini Kristo amemimia Roho juu yenu. Na kufuatana na vile Roho yule anavyokaa ndani yenu, hamuhitaji kufundishwa na mutu, kwa maana Roho wake anawafundisha mambo yote. Roho yule anasema ukweli wala hasemi uongo. Basi kama vile Roho alivyowafundisha, mukae ndani ya Kristo.


Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.


Anawawekea watu wa usawa akiba ya hekima safi, yeye ni ngao kwa watu wanaoishi kwa ukamilifu.


Kwa hiyo muchunge ndani ya mioyo yenu mafundisho muliyosikia tangia mbele. Kama mukichunga mafundisho yale muliyosikia tangia mbele, mutakaa ndani ya Mwana pamoja na Baba.


Zitawaerevusha wajinga, zitawapa vijana maarifa na akili.


Kwa hiyo, utaweza kulinda akili, na kinywa chako kitashika maarifa.


Nina uwezo wa kushauri na kuamua vizuri. Nina ufahamu na nina nguvu.


Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.


Usimwache hekima, nayo itakutunza; umupende, nayo itakulinda.


Anayejipatia hekima anapenda nafsi yake; anayeshika ufahamu atastawi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite