Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 28:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.

Gade chapit la Kopi




Mezali 28:1
26 Referans Kwoze  

Waadui zenu wakiwashambulia, Yawe atawapa ushindi juu yao. Wakikuja kuwashambulia kwa njia moja watawakimbia kwa njia saba.


Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate; wala hawajali Mungu.


Haogopi habari mbaya; moyo wake unasimama imara na anamutegemea Yawe.


Kama vile munavyojua, mbele ya kufika kwenu tuliteswa na kutukaniwa kwanza katika muji Filipi. Lakini ingawa tulipata vizuizo vingi, Mungu alitupatia uhodari wa kuwapasha ninyi Habari yake Njema.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Paulo na Barnaba wakakaa Ikonio kwa muda murefu. Walisema kwa uhodari kabisa, wakimutumainia Bwana. Naye aliwapa uwezo wa kufanya maajabu na vitambulisho. Na kwa njia hiyo alihakikisha kwamba ujumbe walioutangaza juu ya neema yake ulikuwa wa kweli.


Maana, Yawe anasema hivi: Nitakufanya ukuwe kitisho kwako wewe mwenyewe na kwa warafiki zako wote. Wao watauawa katika vita kwa upanga wa waadui zao, wewe ukiwa ukiangalia. Nitawatoa watu wote wa Yuda katika mikono ya mufalme wa Babeli, naye atawapeleka kuwa watumwa mpaka Babeli na kuwaua kwa upanga.


Na kwa njia ya wamoja wenu watakaobaki nitaleta woga ndani ya moyo wao, katika inchi ya waadui zao hata jani linalopeperushwa litawakimbiza. Watakimbia kama mutu anayekimbia vita. Watakimbia na kuanguka hata kama hakuna mutu anayewafukuza.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


Watu hao wakaenda mpaka Yordani na katika njia waliona nguo na vifaa vingine Waaramu walivyoacha walipokuwa wanakimbia. Wakarudi na kumupasha mufalme habari.


Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.


Musa akamalizia kwa kumwambia mufalme: “Watumishi wako hawa watanifikia na kuinama mbele yangu kwa heshima, wakinisihi niondoke katika inchi ya Misri, mimi pamoja na watu wote wanaonifuata. Nyuma ya hayo, nitaondoka.” Kisha Musa, akiwa amekasirika, akaondoka kwa mufalme wa Misri.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”


watakupa maziwa ya kukutoshelea na jamaa yako, na kwa ajili ya wajakazi wako.


Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.


Basi, waalikwa wa Adonia wakaogopa sana, wakaondoka na kutawanyika.


Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio. Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.


Hapo watashikwa na hofu, hofu ambayo hawajapata kuiona; maana Mungu ataitawanya mifupa ya waadui, hao watafezeheka maana Mungu amewakataa.


Anayeishi kwa ukamilifu anaishi salama, lakini anayepotosha maisha yake atagunduliwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite