7 Mezali katika midomo ya mupumbafu ni kama miguu ya kiwete inayoninginia.
Mezali katika kinywa cha mupumbafu ni kama tawi lenye miiba katika mukono wa mulevi.
Maneno mazuri hayastahili katika kinywa cha mupumbafu, zaidi sana maneno ya uongo katika kinywa cha kiongozi!
Lakini Mungu atawapiga mishale, na kuwaumiza kwa rafla.
Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”
Kutuma ujumbe kwa mukono wa mupumbafu ni kama kujikata miguu au kujitafutia mateso.
Kumupa mupumbafu heshima ni kama kufunga jiwe kwenye mujeledi.