Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 26:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kiboko ni kwa farasi, lijamu ni kwa punda, na fimbo ni kwa mugongo wa mupumbafu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 26:3
10 Referans Kwoze  

Katika kinywa cha mwenye ufahamu kuna hekima, lakini wasiokuwa na akili watapigwa fimbo katika mugongo.


Basi munataka nini? Nifike kule kwenu, nikikuja na fimbo au na moyo unaojaa upendo na upole?


Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu, ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa, kama sivyo hawatakukaribia.”


Kwa wakati huu ninapokuwa mbali nanyi, ninarudilia kuwaambia waziwazi maneno yale niliyokuwa nimekwisha kuwaambia mbele katika safari yangu ya pili niliyofanya kwenu. Ninawaambia kwamba nitakapokuja kwenu mara tena, sitakosa kuazibu wale waliofanya zambi zamani na wengine wote.


Sisi tuko tayari kuazibu kila kitendo cha uasi, mutakapoonyesha kwamba munatii kabisa.


Hata kama ukitwanga mupumbafu katika kinu, sawa na ngano, hautaweza kumutenganisha na upumbafu wake.


Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.


Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.


Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite