Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 26:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.

Gade chapit la Kopi




Mezali 26:12
17 Referans Kwoze  

Unamwona mutu anayesema bila kufikiri? Mutu mupumbafu ni afazali kuliko yeye.


Mukuwe na masikilizano kati yenu. Musikuwe na nia ya kujitukuza, lakini mukubali kuishi katika unyenyekevu. Musijiwazie kuwa wenye akili sana.


Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima, lakini masikini mwenye akili atamufichua.


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Umujibu mupumbafu kama kufuatana na upumbafu wake, kusudi asijione kuwa mwenye hekima zaidi.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.


Muvivu anajiona kuwa mwenye hekima kuliko watu saba wanaoweza kujibu kwa akili.


Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi? Yule atawatumikia wafalme; hatawatumikia watu wasiofaa.


Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.


Yesu akawajibu: “Mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini kwa maana munajidai kwamba munaona, mungali katika zambi.”


Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.


Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.


Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite