13 Usiache kufundisha mutoto; ukimupiga fimbo hatakufa.
Asiyemwazibu mutoto wake hamupendi; lakini anayemupenda mwana wake atamwazibu kwa wakati.
Umwazibu mwana wako naye hatakupa wasiwasi; yeye atafurahisha moyo wako.
Azabu na maonyo vinaleta hekima, lakini mutoto aliyeachiliwa anapatisha mama yake haya.
Azibu mwana wako wakati kungali bado tumaini lakini usitafute kumwangamiza.
Muvumilie maadibisho; kwa maana Mungu anawatendea ninyi kama wana wake. Tena, ni mwana gani asiyeazibiwa na baba yake?
Tumia akili yako kwa kufuata mafundisho; tumia masikio yako kwa kusikiliza maarifa.
Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mutoto, lakini fimbo ya kufundisha itaufukuza mbali.