2 Watajiri na wamasikini wana hali hii moja: Yawe ni Muumba wao wote.
Maana Mungu ndiye aliyeniumba mimi na mutumishi wangu; yeye ndiye aliyetuumba sisi wote.
Anayemutesa muzaifu anamutukana Muumba wake, lakini anayemwonea huruma mukosefu anamutukuza Mungu.
Yawe anawafanya wamoja wakuwe wamasikini, na wengine wakuwe watajiri. Anawashusha wamoja, na kuwainua wengine.
Masikini na mugandamizaji wanafanana kwa kitu kimoja: wote wawili wamepewa macho na Yawe.
Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.
Jicho haliwezi kuuambia mukono: “Sina lazima yako!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Sina lazima yenu!”