11 Mwenye nia safi na maneno mazuri atakuwa rafiki wa mufalme.
Heri wale wanaokuwa na moyo safi, maana watamwona Mungu!
Mufalme anapendelea mutu anayesema maneno ya haki. Anamupenda mutu anayesema kwa usawa.
Mufalme anapendezwa na mutumishi anayetenda kwa hekima, lakini hasira yake inawapata wanaotenda mambo yasiyofaa.
Nitawaangalia waaminifu katika inchi, wapate kuishi pamoja nami. Watu wakamilifu, ndio watakaonitumikia.
Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.
Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”
Basi, mufalme Nebukadneza akawapandishia vyeo Sadiraki, Mesaki na Abedenego katika jimbo la Babeli.
Mordekayi, Muyuda, alikuwa wa kwanza chini ya mufalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayuda, maana alitumika kwa faida na amani ya watu wake na wazao wao wote.
Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo.
Yawe analinda maarifa lakini anayavuruga maneno ya waovu.
Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.