5 Mipango ya mutu wa bidii inaleta mali kwa wingi, lakini kila mutu anayetenda kwa harakaharaka anapata umasikini.
Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.
Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.
Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.
Mali iliyopatikana kwa haraka kwa mwanzo, haitakuwa ya heri kwa mwisho.
Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.
Unamwona mutu anayesema bila kufikiri? Mutu mupumbafu ni afazali kuliko yeye.