Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 21:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.

Gade chapit la Kopi




Mezali 21:21
19 Referans Kwoze  

Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Ukinyenyekea na kumwogopa Yawe, utapata zawadi ya fanaka, heshima, na uzima.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini Mungu anawapenda wale wanaofuata mambo ya haki.


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Lakini muchunguze kila jambo na kushika lile linalokuwa jema.


Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


navyo vitakuwa uzima katika nafsi yako, na pambo zuri katika shingo lako.


Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza; yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.


Mushahara wa mutu wa haki ni uzima, lakini mapato ya mwovu ni katika zambi.


Mutu anayekusudia kuwa mwenye haki ataishi, lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite